SHETANI

 Wanyofu hatuamini uwepo wa kiumbe cha kusadikika, shetani. Sababu zote zote zitolewazo kuthibitisha uwepo wa kiumbe huyo wa uongo hazikidhi viwango, kwa sababu kimsingi binadamu ni mwenye uwezo wa kuchagua mema au mabaya kwa hiyo si lazima awepo kiumbe mwingine kumkatisha shauri katika chaguzi zake hizo. Binadamu yeye binafsi ana uwezo wa kuchagua mabaya na yeye huyo huyo anao uwezo pia wa kuchagua mema. Aidha pia matatizo mbali mbali yaliyopo ulimwenguni sio matokeo ya uwepo wa shetani, mfano malaria sio matokeo ya shetani, ni matokeo ya plasmodium, ukiugua Malaria maana yake umeng'atwa na mbu waenezao malaria na shetani kwa vyo vyote hajahusika hapo. Kwa kifupi Wanyofu tunasema uwepo wa matatizo duniani ni matokeo ya uchanga wa Mamlaka ya Nafsi, pamoja na matumizi mabaya ya Mamlaka ya Nafsi.

Uwepo wa kiumbe huyo wa uongo mioyoni mwa watu kumepelekea changamoto nyingine kuongezeka duniani, kwa sababu dini zimekuwa badala ya kuleta amani duniani zimechangia umwagaji damu wa kutisha zaidi kwa sababu kila dini ilimhisi shetani nyuma ya dini nyingine, wakatoliki barani Ulaya wameua mamilioni ya wakristo wacha Mungu kisa tu kanisa liliwaona wazushi yaani wamefuata mafundisho ya shetani , waislamu katika vita zao za jihad, hadi leo matukio ya kujitoa mhanga dini zinahisi zinamtumikia Mungu kwa kuangamiza wafuasi wa shetani. 

Watu badala ya kukaa chini na kutafuta suluhu za kudumu kwa changamoto zao za kiroho, kiakili, kimwili na kiuchumi, ndoa nyingi zinaparanganyika lakini jawabu linakuwa jepesi tu siku zote , dini zinatoa jibu jepesi tu kwamba dunia haitawezekana kutengemaa kwa sababu humu duniani kuna shetani, ambaye anaonwa kuwa na Nguvu kuliko binadamu na kwa hiyo hamna jinsi, hamna Tumaini tena humu duniani. Jitihada zo zote zinaazofanywa na binadamu kujikomboa na umaskini na majanga mbali mbali zinaonekana kama tu kichekesho kwa dini za kale.

(Kwa Maelezo mengineyo ya ziada BOFYA HAPA)
Kwa vyo vyote uwepo wa shetani ni simango kwa Mungu na ni kama kuonesha kwamba hajui kupangilia na kwamba anazidiwa hekima na sisi viumbe wake, maana awezaje kumtupa humu duniani kama vitabu vinavyosema au hata kumruhusu kiumbe wa hatari, mwenye nguvu kuliko sisi kumruhusu aje humu baada ya kushindikana mbinguni? Kisha sababu ya udhaifu wetu mbele ya kiumbe huyo ikabidi tuanguke licha ya kutopenda kufanya hivyo, lakini tena Mungu huyo huyo aamue kutuchoma moto usio na mwisho, milele na milele na milele, na milele na milele, na milele--Mungu mwenye maamuzi ya hivyo kwa vyo vyote hana upendo wala hekima wala uadilifu.
(BOFYA HAPA kusoma zaidi KUHUSU WANYOFU).

No comments:

Post a Comment